
klabu ya Bournemouth inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza wamemsajili beki wa kushoto wa Chelsea Nathan Ake kwa mkopo na ataitumikia klabu hiyo katika msimu wa mwaka 2016/2017, Ake aliyeitumikia klabu ya Watford msimu uliopita na kucheza kwa kiwango cha juu na kufanikiwa kushinda tuzo ya mchezaji bora mdogo wa mwaka katika tuzo za ndani ya klabu. Ake ameichezea Chelsea mechi 12 alifanikiwa kucheza kwenye mechi za Europa league,pia Ake alisajili mkataba wa miaka mitano na Chelsea msimu uliopita na anaitumikia timu ya taifa ya uholanzi chini ya miaka 21.


No comments:
Post a Comment