Climb the mountains
Kocha wa Chelsea alitumia mkutano wake wa kabla ya mechi na waandishi wa habari kuwaomba mashabiki wa Chelsea wasimzomee mshambuliaji wao Diego Costa kwenye mechi dhidi ya Hull City ambayo amepanga kumrudisha kwenye kikosi cha kwanza. Conte alisema Costa ni mchezaji anayejituma sana anapokua amevaa jezi ya Chelsea. Costa aliachwa kwenye mechi dhidi ya Leicester wiki iliyopita baada ya kugombana na makocha na kususia mazoezi akishinikiza klabu imuuze kwenda China,hata hivyo inaonekana mshambuliaji huyo ataondoka klabuni hapo mwisho wa msimu wakati wa dirisha kubwa la usajili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment