Baada ya kutangaza kustaafu kiungo bora kabisa kupata kutokea Uingereza na klabu ya Chelsea Frank Lampard amerudi rasmi Chelsea kwa ajili ya kuanza safari yake mpya ya ukocha. Frank lampard amepangwa kwenye Academy ya vijana wa Chelsea inayotumia uwanja wa Cobham ambapo kupitia huko ataifukuzia lesini ya ukocha yenye hadhi ya (UEFA B Coaching Licence) kwa mafunzo ya darasani na uwanjani.
Frank Lampard ambaye amecheza mpira kwa Takribani miaka 21 akizitumikia timu za West Ham,Chelsea,Manchester City na New York City FC alitundika daluga akiwa na miaka 38 huku akiwa amefanikiwa kushinda mataji 11.



No comments:
Post a Comment