Blog ikuleteayo habari mbali mbali kutoka klabu ya Chelsea kwa lugha ya kiswahili.

Climb the mountains

Post Page Advertisement [Top]



Kombe la FA limekua la kuvutia sana msimu huu huku likileta matokeo yasiyotarajiwa kwa baadhi ya klabu za ligi kuu kulazimishwa sare/kufungwa na kutolewa na timu zisizoshiriki ligi kuu wala ligi daraja la kwanza. Baada ya matokeo ya mechi za jana FA walifanya droo kupata mechi za robo fainali huku klabu ya Chelsea ikipewa Manchester United na Chelsea atakua mwenyeji wa mechi hiyo hivyo watamkaribisha kocha wao wa zamani Jose Mourinho darajani kwa mara nyingine. Mara ya mwisho Man u alipokutana na Chelsea aliambulia kipigo cha magoli matatu kwa bila,ila hivi sasa itakua ni mechi ngumu kwa wote huku Chelsea akijaribu kuchukua makombe yote mawili yani FA na EPL,mshindi wa mechi hiyo atafuzu kucheza nusu fainali.

No comments:

Post a Comment

Bottom Ad [Post Page]

| Designed by Colorlib