Blog ikuleteayo habari mbali mbali kutoka klabu ya Chelsea kwa lugha ya kiswahili.

Climb the mountains

Post Page Advertisement [Top]

Charlie WakefieldChelseaChelsea Under 18Jaguar XEKinda wa chelsea ampa baba zawadi ya gari

Kinda wa Chelsea amshtukiza baba yake na zawadi ya gari aina ya Jaguar XE lenye thamani ya milioni 70.(PICHA)


Kinda wa Chelsea Charlie Wakefield mwenye  umri wa miaka 18 aliamua kumshtukiza baba yake ambaye alikua anatimiza miaka 50 ya kuzaliwa kwa kumpa zawadi ya gari aina Jaguar XE lenye thamani ya £25,000 sawa na milioni 70 za kitanzania. Charlie ni moja ya wachezaji makinda wenye kiwango cha juu kabisa katika academy ya Chelsea akiisaidia Chelsea Under 18 na under 21 kushinda makombe kama FA na UEFA Youth Leagua mara mbili mfululizo alifanikiwa kusaini mkataba wake wakua mchezaji wa kulipwa akiwa na miaka 17 tuu, Charlie alimuelezea baba yake kama mtu muhimu sana katika Maisha yake ya soka kwani hajawahi kukosa kwenda kumuangalia katika  mechi hata moja tangu akiwa na miaka 8 na muda mwingine ilimlazimu baba yake kundesha gari kwa masaa 6 ili tuu kwenda kumuangalia akicheza,alisema baba yake alikua akitumia gari aina Ford Focus la mwaka 2003 ambalo alinunua likiwa limeshatumika tayari. Alisema amempa Jaguar kwa sababu ni gari ambalo baba yake amekua na ndoto ya kununua muda mrefu  na kwa  sasa ndio gari lililokua ndani ya uwezo wake kulinunua.



No comments:

Post a Comment

Bottom Ad [Post Page]

| Designed by Colorlib