Blog ikuleteayo habari mbali mbali kutoka klabu ya Chelsea kwa lugha ya kiswahili.

Climb the mountains

Post Page Advertisement [Top]

AFC BournemouthChelseaJohn TerryMLSStoke Citywest bromWest Brom want John Terry

West Brom wamesema watajaribu kumsajili John Terry mwisho wa msimu


Kocha wa West Brom Tony Pulis  aviambia vyombo vya habari kua klabu yake itajaribu kumsajili John Terry kwa mara ya pili mwishoni mwa msimu baada ya jitihada zao kumsajili wakati wa dirisha dogo kugonga mwamba,Tony Pulis alisema "Nimekua naamini Terry ni moja ya wachezaji bora kabisa kupata kutokea na ni moja ya wachezaji tuliojaribu kuwasajili mwezi January lakini hatukufanikiwa nadhani aliamua kubaki Chelsea kwa sababu wanafukuzia ubingwa wa Uingereza na yeye kwake itakua heshima kama ataondoka akiwa bingwa" Terry ambaye amecheza mechi moja tuu ya ligi kuu tangu mwezi wa 9 mwaka jana mkataba wake unaisha msimu huu hivi karibuni alipofanya mahojiano na chombo kimoja cha habari aliweka wazi kua amekua na ndoto za kucheza ligi ya Marekani kabla hajasataafu kucheza soka la kulipwa. Ukitoa West Brom klabu za Stoke City na Bournemouth ni klabu zinazomfukuzia mkongwe huyo wa Chelsea.

No comments:

Post a Comment

Bottom Ad [Post Page]

| Designed by Colorlib