Wakati mashabiki wa Chelsea wakisubiria kwa hamu timu yao ya wakubwa ijitangaze kua ni bingwa wa ligi kuu ya Uingereza timu yao ya watoto Chelsea Under 18 walikua wameshajitangaza mabingwa kwenye ligi yao baada ya kumchapa Reading magoli 3 kwa bila. Hivyo kwa siku ya jana Chelsea walikua wakisherekea ushindi mkubwa kwani timu zao zote zilifanikiwa kutwaa ubingwa. Kwa kikosi cha timu ya wakubwa kilichokua kikicheza dhidi ya West Brom ushindi haukuja kirahisi licha ya mara zote kumiliki mpira zaidi ya asimilia 70 goli pekee la Michy Batshuayi alilofunga dakika ya 83 liliweza kuipa Chelsea ubingwa,licha ya mchezaji huyo kucheza mechi chache msimu huu aliweza kugeuka shujaa siku ya jana.





No comments:
Post a Comment