Climb the mountains
ArsenalChelseaChelsea Tour 2017ChinaDiego CostaInter MilanJuventusNemanja maticSingapore
Chelsea kuwaacha Costa na Matic wanapoenda China na Singapore ili waakamilishe utaratibu wa kuhamia klabu nyingine.
Tovuti ya Skysport wameripoti kua Chelsea inategemea kwenda kwenye tour yao bila Costa na kiungo Nemanja Matic sababu kubwa ni ili wachezaji hao wawili wakamilishe utaratibu wa kuhama klabu. Costa ambaye alipewa ruhusa ya kutokuhudhuria mazoezi ya Chelsea wiki nzima wakati klabu ikiendelea kuongea na timu zinazotaka kumnunua wakati Nemanja Matic alirudi pamoja na wachezaji wengine kuanza mazoezi ya mwanzo wa msimu ila kwa sasa wanategemea kumuuza Matic mapema wiki inayokuja huku timu kama Manchester United,Arsenal na Juventus zikifukuzia saini yake. Chelsea wanategemea kwenda kwenye tour nchi ya China na Singapore ambako pia watacheza mechi za kirafiki na klabu za Arsenal,Bayern Munich pamoja na Inter Milan.
Tags: Arsenal
, Chelsea
, Chelsea Tour 2017
, China
, Diego Costa
, Inter Milan
, Juventus
, Nemanja matic
, Singapore
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment