Baada ya Antonio Conte kusaini mkataba mpya habari njema zinaendelea kusikika masikioni mwa mashabiki wa Chelsea kwani Chelsea wamefikia makubaliano na klabu ya Real Madrid kumsajili mshambuliaji Alvaro Morata kwa ada ya paundi milioni 75. Katika kuthibitisha hilo zaidi mwandishi wa habari za michezo wa Daily Telegraph alisema amedokezwa na mtu wake wa karibu anayefanya kazi ndani ya Madridi kua uhamisho wa Morata umeshakamilika. Ikiwa Chelsea watakamilisha usajili wa Mhispania huyo watakuwa wamevunja rekodi yao ya usajili ya paundi milioni 50 walizotumia kumsajili Fernando Torres.
No comments:
Post a Comment