Chelsea alikua kwenye nafasi nzuri sana ya kumsajili Bakayoko mwishoni mwa mwezi wa sita lakini wameshindwa kufanya hivyo mpaka sasa,huku klabu ya Manchester United nao wakituma ofa Monaco kumsajili mchezaji huyo mashabiki wengi wa Chelsea wanapata hofu isije wakazidiwa kete kama walivyozidiwa ka Lukaku.Chelsea wanashindwa kukamilisha usajili huo sababu Bakayoko ana matatizo ya kifundo cha mguu yanayomsumbua tangu mwezi wa pili na inasemekana nyota huyo atahitaji upasuaji ili kurekebisha tatizo hilo na upasuaji unaweza kumuweka nje ya uwanja kwa wiki 8 mpaka 10,mwanzo wa msimu Chelsea wanategemea kumkosa nyota wao Eden Hazard sababu ya majeruhi hivyo wanaamini wanahitaji kuimarisha idara nyingine zote ili kuanza msimu vizuri na ndio kitu kinachowapa viongozi wasiwasi kumsajili nyota mwingine ambaye ni majeruhi.
No comments:
Post a Comment